WACHEZAJI SINGIDA UNITED WAZIVAA ADHABU ZA TFF MECHI YA FA DHIDI YA GREEN WORRIOURS

Kamati ya mashindano ya Shirikisho la Soka nchini TFF imewafungia mechi tatu za Kombe la Shirikisho (FA) Mshambuliaji wa Singida United Deus Kaseke na Mlinda Mlango wa Green Warriors Shaaban Dihile pamoja na faini ya Shilingi laki Tano kila mmoja huku Kambale Salita “Papy Kambale” wa Singida naye akipelekwa kwenye kamati ya Nidhamu.


Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF Efrem August amesema, Kamati ilikutana Februari 13 mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine ilipitia taarifa za mchezo huo ambapo ilionyesha kuwa Kaseke na Dihile hawakuingia uwanjani na timu zao na hawakuwepo wakati timu hizo zikipeana mikono Uwanjani.

Wachezaji Deus Kaseke na Shaaban Dihile wamefungiwa mechi tatu pamoja na faini ikiwa ni kwamujibu wa kanuni za Kombe la Shirikisho Kanuni 31 kifungu cha kwanza ambayo inaelezea kwamba kwa kosa hilo wachezaji waadhibiwe kulingana na kanuni ya Ligi husika ambapo tukienda kwenye kanuni ya Ligi kuu ambapo Singida wanashiriki, kanuni namba 37 kifungu cha 7 D kinaelekeza kwamba mchezaji afungiwe mechi tatu na Faini ya Shilingi Laki 5, kwahiyo hawatashiriki mechi tatu za Kombe la Shirikisho, ” amesema.


Efrem ameongeza kuwa, Papy Kambale aamepelekwa kwenye kamati ya Nidhamu ay TFF kwa kosa la kumpiga mchezaji wa timu pinzani kwenye mchezo uliozikutanisha timu hizo Januari 31mwaka huu Uwanja wa Azam Complex Chamazi ambapo kamati ya Nidhamu ya TFF itatoa maamuzi zaidi kuhusu kosa lake.

 Wachezaji wa Singida United
   Mudathir Yanya na Deus Kaseke
                                    

No comments