MSA

 
Mugeta Soccer Academy(MSA)ni kituo cha kulea na kukuza vipaji kwa vijana vile vile MSA ukiachilia mbali kukuza vipaji kwa vijana tunalojukumu la kuwapa malezi bora vijana wetu kwa kuwapa uangalizi makini kuanzia majumbani hadi mashuleni kwa kufuatilia maendeleo yao kitaaluma hadi kinidhamu.
MSA pia ni kama mlezi kwani tunaona vijana ambao family zao hazina uwezo wa kuwapeleka shule ama kuwasaidia mahitaji ya maalum shuleni hivyo MSA tunabeba jukumu hili na kuweza kuwasaidia vijana wetu ili kuhakikisha wanafanya izuri kote kote kiwanjani pamoja na shuleni.
Tunao vijana wa umri mbalimbali katika kituo chetu wale wa U12,U14,U16 na U17.Malengo yetu makubwa ni kutengeneza kizazi cha soka kitakachokuwa tegemeo kwa taifa na bara letu.
Kituo chetu kimeanzishwa rasmi mwaka 2016 chini ya maono ya mwanasoka wa kitanzania anayechezea nchini ujerumani Emily Mugeta.Makao makuu ya MSA ni wilayani Ukerewe mkoani Mwanza.

No comments