MAYANGA ASEMA HAWAHOFII ALGERIA HATA KAMA WALISHAWAHI KUFUNGWA 7-0, NA HICHI NDICHO WANACHOKIHITAJI LEO

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” kimesema licha ya kuwa na historia mbaya ya kufungwa na Algeria bao 7-0 lakini leo kimejipanga kwaajili ya ushindi dhidi ya wapinzani wao hao ikiwa ni mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa kalenda ya FIFA utakaopigwa mjini Algiers, Algeria ili kupanda katika viwango vya FIFA.

Kocha Mkuu wa Timu hiyo Salum mayanga amesema, kikosi kipo imara kwaajili ya mchezo huo utakaopigwa majira ya saa mbili usiku kwa saa za hapa nyumbani na wanaamini kutokana na maandalizi waliyonayo japo niyamuda mfupi lakini yataweza kuwapa matokeo mazuri ndani ya Dakika 90.

“Timu ya Taifa stars ipo kwenye hali nzuri tangu jana tulipomaliza mazoezi jana na leo tunajiandaa kabla ya mechi yetu ambayo itachezwa majira ya saa 12 jioni kwa saa za huku Algreria na kwatanzania ikiwa ni saa mbili usiku, ” amesema.

“Nimatumaini yetu tutacheza mchezo mzuri na kuweza kupata ushindi katika mchezo wa leo jambo ambalo litakuwa zuri kwetu, kwakifupi kila mchezaji anamorali na tutakapomaliza mchezo huo, kesho timu itaanza safari yakurejea nyumbani, ” amesema.

Kikosi cha Taifa Stars kinahistoria mbaya na Algeria mara baada ya Novemba 17 mwaka 2015 kupokea kipigo cha bao 7-0 katika mchezo wake wa pili wa marudiano ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi kikosi kikiwa chini ya Kocha Boniface Mkwasa.
Kikosi cha Timua ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars"

No comments