KMC YAIPANIA AZAM FC KESHO ASFC, YASEMA HAWAHOFII WACHEZAJI WAO WAKIMATAIFA
Hatua
ya 16 bora mzunguko wa Nne wa mashindano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) inaendelea kesho kwa michezo miwili kupigwa ambapo KMC
ambao watakuwa wenyeji wa Azam FC Majira ya saa Moja jioni wamesema
hawatishiki na uwezo wa wapinzani wao kwani wanajiamini katika uwezo
wa kupambana.
Akizungumza
mara baada ya kumaliza mazoezi Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam,
Kocha wa KMC Fredy Felix Minziro amesema, mchezo dhidi ya Azam FC
wanauchukulia kwa uzito wa hali ya juu kwani licha ya kutafuta
matokeo mazuri lakini pia anaangalia uwezo wa wachezaji wake kutokana
na uzoefu walionao wapinzani wao.
“Hii
mechi naichukulia kwa uzito mkubwa kwa sababu nawaheshimu Azam FC, ni
timu kubwa na imefanya usajili zuri na hata kwenye Ligi kiwango chao
ni kizuri lakini KMC ndio kwanza tumepanda kushiriki Ligi kuu kwa
msimu ujao na Azam wapo kwenye Ligi kuu kwa kipindi kirefu kwahiyo
mechi hii itakuwa ni kipimo tosha kwetu kuangalia kwamba uwezo wa
timu yetu upo vipi, ” amesema.
Kocha
Minziro amesema, ameshawahi kuwaona Azam FC mara nyingi wakicheza na
hajaona tofauti ya wachezaji alionao na wale wa Azam FC japo
wapinzani wao wanawachezaji wa Kimataifa na wenye uwezo lakini hawezi
kuhofia huku akiongeza kuwa kufanya vizuri kwenye ASFC ni chachu au
mafanikio ya kupanda kushiriki Ligi kuu msimu ujao ndio umewapa nguvu
ya kuweza kufanya vizuri kwenye FA.
“Nawaamini
sana vijana wangu a sioni tofauti na wale wa Azam FC japo
wanawachezaji wa Kimataifa na wenye uwezo lakini bado sina hofu nao
na naimani kubwa sana na vijana wangu hivyo kubw ani kuwaomba
mashabiki waweze kuja Chamazi kesho kwaajili ya kutupa sapoti kama
walivyokuwa wakifanya katika mechi zilizopita naamini tutasonga mbele
katika michuano hii, ” amesema.
Kwaupande
wake Beki wa Timu hiyo Juma Jabu amesema, kila mchezaji anajua jukumu
alilonalo katika mchezo huo na wanawaheshimu wapinzani wao japo lengo
kubwa lililombele yao ni kusonga mbele katika michuano hiyo.
“Muda
hatuna tatizo nao kwani hakuna kuwa na jua na hali ya hewa itakuwa
nzuri, kila mchezaji naamini kajipanga vizuri kwaajili ya kuweza
kupambana, Azam ni timu kubwa na inawachezaji wenye uwezo mzuri
lakini sisi tumejipanga kupambana na kuweza kushinda katika mchezo
huo ili tusonge mbele, ” amesema.
Mbali
na mchezo huo, mchezo mwingine utakaopigwa hapo kesho ni Singida
United ambao watawakaribisha Polisi Tanzania Uwanja wa Namfua Mjini
Singida huku Mzunguko huo wa Nne(4) utaendelea tena Jumapili Februari
25, 2018 kwa Buseresere kuwaalika Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa
Nyamagana Mwanza mchezo utakaochezwa saa 8 mchana wakati Majimaji FC
ya Ruvuma watakuwa nyumbani kwenye uwanja wa Majimaji kuwakaribisha
Young Africans ya Dar es Salaam mchezo ukichezwa saa 10 jioni nao
Ndanda FC watakuwa ugenini kucheza na JKT Tanzania Azam Complex
Chamazi saa 1 usiku.
Mzunguko
huwa wa 4 utakamilika Jumatatu Februari 26, 2018 Kiluvya United dhidi
ya Tanzania Prisons saa 8 mchana Uwanja wa Mabatini na Stand United
watawaalika Dodoma FC saa 10 jioni uwanja wa Kambarage.
KMC katika moja ya mchezo wa Kirafiki waliokutana na Azam FC Uwanja wa Chamazi
Post a Comment