MUDA WA WAJUMBE WA MKUTANO WA FIFA TANZANIA KUANZA KUWASILI SIKU HII.
Wajumbe wanaotarajia kushiriki
mkutano wa Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA wanatarajia Kuanza kuwasili
kesho kwaajili ya mkutano huo utakaofanyika Februari 22 Ukumbi wa Mwalimu
Nyerere Jijini Dar es salaam.
Afisa Habari wa Shirikisho la soka
nchini TFF Mario Clifford Ndimbo amesema, maandalizi kwaajili ya mkutano
huo yameshakamilika na wanaendelea na mawasiliano ili kujua Rais wa FIFA ambaye
atawasili na ndege na ndiye mjumbe wa mkutano huo atawasili lini na muda gani.
"Rais anawasili kwa ndege
binafsi kwahiyo tunafanya mawasiliano kujua siku na muda rasmi atakaowasili,
na maandalizi yameshakamilika hivyo tunatarajia kila kitu kitakwenda kama
kilivyooangwa, " amesema.
Wakati huohuo TFF kupitia kwa afisa
Habari wake Mario Clifford Ndimbo amesema, mara baada ya ungwe ya Kwanza
ya uuzwaji wa tiketi za kushuhudia Kombe la Dunia, FIFA imeongeza tiketi kwa
mashabiki watakaohitaji kushuhudia Fainali hizo zitakazofanyika Mwezi Juni
mwaka huu nchini Russia.
“Shirikisho la Soka Ulimwenguni
(FIFA) limetuongeza tiketi Tanzania za kushihudia mechi za Kombe la Dunia mwaka
huu pale Russia, ikumbukwe kuwa mwanzoni Tanzania tuliletewa tiketi 290 kabla
ya zoezi kuweka kufungwa Mwezi Januari, lakini sasa wametufungulia ungwe
nyingine ya tiketi hizo kwa maana kwamba kwa Matanzania yoyote anayetaka
kushuhudia Fainali hizo za Kombe la Dunia basi awasiliane na Idara ya
mashindano ya TFF na ungwe hii inataraji kumaliziak Machi 12 mwaka huu kwamaana
zoezi litafungwa, ” amesema.
Post a Comment