ANACHO KIJUTIA GIROUD TANGU ALIPO ONDOKA ARSENAL NI HIKI.

Mshambuliaji Olivier Giroud amesema ameondoka Arsenal akiwa anajutia kitu kimoja tu, kushindwa kubeba taji la Ligi Kuu England akiwa na miamba hiyo ya Emirates.


Mshambuliaji huyo Mfaransa kwa sasa yupo Chelsea alishinda mataji matatu tu ya Kombe la FA alipokuwa na kikosi cha Arsenal kabla ya kutimkia Stamford Bridge kwenye dirisha lililopita la usajili kwa ada ya Pauni 18 milioni ili kupata nafasi ya kucheza akaitumikie Ufaransa kwenye Kombe la Dunia.

Kwenye mahojiano aliyofanyiwa na mchezaji wa zamani wa Chelsea na Arsenal, ambaye pia ni Mfaransa mwenzake, William Gallas, kwamba anajutia nini baada ya kuondoka Emirates, Giroud alisema: “Kujutia? Ni jambo lilelile lililozoealeka, si gumu kulifikiria.

“Sijui kama hiyo ni kujutia au vipi, lakini nasikitika kumaliza maisha yangu kwenye kikosi cha Arsenal bila ya kutwa taji la Ligi Kuu England kitu ambacho ndiyo lengo la kwenda kujiunga na timu hiyo.

“Sawa unaweza kusema juu ya muda kwamba ni mchache, lakini hiyo ndiyo ilikuwa dhamira yangu. Hata hivyo ndoto hazijafutika, bado nipo kwenye Ligi Kuu England na sasa nipo Chelsea.”

No comments