HIKI NDICHO ANACHOKIAMINI MSUVA MARA BAADA YA BENCHI LA UFUNDI LA TAIFA STARS KUFANYA ONGEZEKO LA WACHEZAJI WANAOCHEZA LIGI YA ZANZIBAR

Winga wa Kimataifa Mtanzania anayeitumikia Klabu ya Difaa El Jadida ya nchini Morocco Simon Msuva amesema uamuzi wa benchi la ufundi la Timu ya Taifa ya Tanzania kufanya ongezeko kwa kuchukua wachezaji wanaocheza Ligi ya Zanzibar ni mzuri na wanaamini watashirikiana ili kuweza kuipa timu ya taifa matokeo mazuri katika michezo ya Kirafiki ya Kalenda ya FIFA dhidi ya Algeria na DR Congo na hata katika mashindano mbalimbali.




Msuva amesema kuwa, anaimani na wachezaji wa Zanzibar kwani kwa kushirikiana wataweza kuitangaza zaidi Tanzania katika ramani ya Soka.


Msuva amesema, anaamini benchi la ufundi lilikaa na kuangalia uwezo wa wachezaji waliowachagua kwani kila mchezaji anauwezo na wanaamini hata katika timu watakazokutana na zo wataweza kufanya vizuri zaidi.


Msuva amesema, Timu ay Taifa ni yawachezaji wote na hata kama mchezaji ajaitwa katika kikosi hana haja ya kukata tamaa kwani kila mchezaji anamuda wake wa kuchezea timu ya Taifa kikubwa ni kufanya jitihada katika vilabu ili waweze kuonekana.


Msuva ameongeza kwa kuwataka wachezaji wa hapa nchini kuongeza jitihada katika soka na kutokukata tamaa ili kuweza kutoka nje ya mipaka ya Tanzania kwaajili ya kukuza soka lao kwamanufaa ya timu ya Taifa.


Msuva amesema, hiki ndicho kipindi cha wachezaji wengi zaidi kutoka kwaajili ya kucheza soka la kulipwa kwani wanapofanikiwa kutoka wachezaji wengi inasaidia kwa kiasi kikubwa timu ya Taifa kuweza kufanya vizuri kwani inakuwa na wachezaji wazuri na wenye viwango.

    Winga wa Kimataifa anayeitumikia Klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco                                                               Simon Msuva

Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi. 

No comments