CHUJIO KUPITA TENA NGORONGORO HEROES MARA BAADA YA KUMALIZANA NA MOROCO KESHO PAMOJA NA MSUMBIJI MACHI 21
Kikosi
cha Timu ya Taifa ya vijana walio na umri chini ya Miaka 20
“Ngorongoro Heroes” kesho kinashuka dimba la Uwanja wa Taifa
jijini Dar es salaam kuvaana na Timu ya Taifa ya Taifa ya Moroco
katika mchezo wa kwanza wa Kirafiki ikiwa ni maandalizi kwaajili ya
kuwania kufuzu AFCON U20.
Kocha
Ninje amesema, mchezo huo pamoja na ule dhidi ya Msumbiji utakaopigwa
Machi 21 utatumika kama mchujo wa kupata kikosi cha wachezaji angalau
23 watakaoweza kuanza maandalizi ya mbio za kuelekea katika michuano
ya AFCON ambapo mchezo wa kwanza wataanza dhidi ya DR Congo Machi 31
katika uwanja wa Taifa kabla ya ule wa marudiano utakaofanyiika baada
ya wiki mbili jijini Kinshansha.
“Kikosi
kipo imara na leo tunafanya mazoezi ya mwisho kwaajili ya maandalizi
ya mchezo wa kesho, Tumepata michezo miwili ya Kimataifa na ni vizuri
kwenda kwenye mashindano makubwa ikiwa umeshaona kikosi chako
kinavyocheza kwahiyo nashukuru sana na nategemea kuwajua vizuri
wachezaji wangu na nitajua nitumie vijana wangapi katika mchezo wa
Congo, ” amesema.
Kikosi cha Ngorongoro Heroes
Kocha
Ninje amesema, mpaka sasa anakikosi cha wachezaji 30 kwahiyo hawezi
kwenda na wachezaji wote bali anachagua vijana angalau 23 ambao
anaamini wataweza kuanza kampeni za kuwania kushiriki AFCON.
“Nitajaribu
kuangalia katika kikosi cha kesho na kwenye mchezo dhidi ya Msumbiji
pia nitaangalia halafu tutakaa na kuangalia wachezaji wapi
tuwapunguze lakini sio kwa mabaya kwani tutawapunguza waende kwenye
klabu zao lakini muda wowote pia tutaweza kuwatumia, ” amesema.
“Kila
mchezaji yupo vizuri kwahiyo najua tutapata wakati mgumu katika
kuchagua wachezaji hao ninaowahitaji ila vipo vigezo pia, ”
amesema.
Kocha
Ninje amesema, kikosi amekikuta kikiwa katika hari nzuri ya kupambana
hivyo imempa urahisi pia wa maandalizi kwaajili ya michezo iliyopo
mbele yao.
Kocha wa Ngorongoro Heroes, Amy Ninje
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Post a Comment