CHAMA CHA RIADHA TANZANIA (RT) KIMETAKIWA KUSITISHA TOZO HII NA BARAZA LA MICHEZO TANZANIA.



Baraza la michezo nchini (BMT) limekiagiza Chama cha riadha Tanzania (RT) kusitisha tozo la ada mpya za mbio ndefu (Marathon) na itumike ada ya zamani ili kuepisha kutokuelewana baina ya waendeshaji wa mbio hizo na RT. 


Katibu mkuu wa BMT Mohamed Kiganja amesema,  mara baada ya RT kukutana na wadau wa Marathon Oktoba mwaka jana na kuwaelekeza mabadiliko ya ada kulitokea sintofahamu baina yao na kupelekea waendeshaji wa Marathon kuandika barua serikalini wakilalamikia ongezeko la ada ambalo lilipanda mara mbili hivyo wao wakiwa ni Serikali imewalazimu kutoa uamuzi huo huku wakipanga kukutana na wadau pamoja na chama ili kutengeneza namna bora ya kuratibu mbio hizo. 

"Waendeshaji wa Marathon walikiwa wakilipa baadhi ya mbio kiasi cha shilingi milioni mbili na zikapanda mpaka milioni sita,  kwahiyo kama Serikali hatuwezi kulifumbia macho na tunaamini maamuzi haya tunaamini hakutokuwa na migogoro isiyo na sababu, " amesema. 

Kiganja amewataka waandaaji wa mbio hizi kuwa mara baada ya kusitoshwa ada mpya wanatakiwa kufuata sheria kwani wengi wao bafo hawajasajiliwa. 

Kiganja ameongeza kuwa Machi 05 mwaka huu mara baada ya kumalizika kwa mbio za Kili "Kili Marathon" watakutana pande zote wakiwemo BMT, RT na waandaaji ili kujadili suala hilo. 

Kiganja ameongeza kwa kuwataka waandaaji wote kutumia kamati za michezo za mikoa kama sheria zinavyotaka

No comments