Simba Wamepewa Mapumziko Ya Muda Huu Kutofanya Mazoezi
Kikosi cha vinara wa michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC
kimepewa mapumziko mafupi ya siku moja, kutofanya mazoezi baada ya
kumaliza mchezo wao wa kimataifa.
Taarifa
hiyo imetolewa na uongozi wa timu hiyo mchana wa leo kupitia ukurasa
wao maalumu wa facebook huku wakidai wanatarajia kusafiri alfajiri ya
kesho kuelekea mkoani Shinyanga.
Kwa upande mwingine, timu ya Simba imerejea katika mashindano ya kimataifa kwa kishindo baada ya kuichapa Gendarmerie ya Djibouti kwa mabao 4-0 katika raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika, mchezo uliofanyika (jana) Jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kwa upande mwingine, timu ya Simba imerejea katika mashindano ya kimataifa kwa kishindo baada ya kuichapa Gendarmerie ya Djibouti kwa mabao 4-0 katika raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika, mchezo uliofanyika (jana) Jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Post a Comment