USHINDI DHIDI YA GENDARMERIE HAINA MAANA KWAMBA TUMEVUKA, TUNAKAZI NGUMU DJIBOUT - SIMBA SC
Mara
baada ya kuibuka na ushindi wa bao 4-0 dhidi ya Gendarmerie Tnale
hapo jana katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza ya Kombe la
Shirikisho Afrika, Uongozi wa Klabu ya Simba umesema ushindi huo
haumaanishi kwamba wameshavuka katika hatua hiyo kwani mchezo wa
marudiano ni mgumu na unahitaji taahadhari kubwa.
Mkuu
wa
Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba
SC
Haji Manara amesema, bado hawajafuzu kwa mzunguko unaofuata bali
wameshinda mchezo wa dakika 90 hivyo bado 90 zilizobakia na hata
wapinzani wao ni timu nzuri ambayo inaonyesha wanaweza kufanya vizuri
zaidi katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Februari 20 nchini
Djibout.
“Bado
mechi haijaisha, hatujafuzu bado kwa mzunguko unaofuata kwasababu
mechi hizo ni dakika 180 nyumbani na ugenini, mechi ya nyumbani
tumeshinda bado ya ugenini, kwahiyo tunaangalia mechi ya ugenini
itakayochezwa Djibout, ” amesema.
Manara
amesema, timu waliyokutana nayo ni nzuri na yenye kucheza kwa
kuheshimu mchezo na wanaamini wanaweza wakaona mchezo mzuri zaidi wa
wapinzani wao zaidi ya ule walioucheza hapo jana.
“Sio
timu mbaya kama watu wengi wanavyodhani na jana tumeona, wanacheza
kwa kuzia sana na wamejitahidi, bila shaka wanaweza wakafunguka
wakiwa kwao na hapo tunaweza tukaona mchezo mzuri zaidi kuliko
tuliouona jana, ” amesema.
Wakati
huoho Manara ameongeza kuwa, Kikosi kamili cha wachezaji wa Klabu ya
Simba kinatarajia kuondoka kesho kuelekea Mjini Shinyanga kwaajili ya
maandalizi ya mchezo dhidi ya Mwadui FC utakaopigwa Alhamisi ya wiki
hii huku wakimkosa beki wao Mghana ambaye anamiliki kadi tatu za
njano pamoja na wachezaji ambao bado ni majeruhi ndani ya kikosi
hicho.
“Tunakwenda
na Kikosi kamili Shinyanga, tunatarajia kumkosa Asante Kwasi
kwasababu anakadi tatu za njano, pia wachezaji waliokuwa na majeraha
ya muda mrefu ambao sasa wameshaanza kufanya mazoezi, lakini tukirudi
kutoka Shinyanga tutataja timu kamili itakayoondoka kuelekea Djbout
lakini bila shaka tutaondoka na timu yote kwa sababu unajua ratiba ni
ngumu kwahiyo tukitoka Djibout tunakutana na mechi ya Ligi hapa na
Mbao kwahiyo hatuwezi kuwaacha wachezaji katika safari ya Djibout, ”
amesema.
Simba
SC ilipata ushindi wa bao nne kupitia kwa kiungo Said Hamisi Ndemla,
Nahodha na mshambuliaji John Raphael Bocco aliyefunga magoli mawili
na mshasmbulaiji Mganda, Emmanuel Arnold Okwi.
Post a Comment