TAMASHA LA SOKA LA WANAWAKE “LIVE YOUR GOALS” KUFANYIKA FEBRUARI HII MJINI KIGOMA



Tamasha la Soka la wanawake linalotambulika na Shirikisho la soka uliwenguni FIFA ambalo linafahamika kama “LIVE YOUR GOALS”  linatarajia kufanyika Jumapili ya Februari 25 mesma huu Mjini Kigoma huku ikienda sambamba na ufunguzi wa Ligi kuu ya wanawake inayofahamika kama Super 8.



Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la soka nchini (TFF) Salum Madadi amesema,  tamasha hilo lenye lengo la kutoa taswira njema ya soka la wanawake Duniani litashirikisha wakimbizi kutoka kambi mbalimbali zilizopo kigoma. 

"Tamasha hili limepewa jina na FIFA linaitwa Leave your goal, na linakusudia kutoa taswira njema ya mpira wa kinamama Duniani, sasa sisi tumepanga kufanyia Kigoma na hili litakiwa la aina yake kidogo kwa maana tunawashirikisha wakimbizi kutoka kwenye makambi yaliyopo Kigoma, " amesema. 

Madadi amesema Tamasha hilo limeungamishwa na mambo mengine mawili yakiwemo kozi ya Grassroot ambayo itaanza kesho na kuhitimishwa siku ya Tamasha hilo huku siku hiyo ya wanawake yaani Super 8 itakayoanza Februari 24 ikizinduliwa Februari 25 kwa mechi ya ufunguzi ya Sisters ya Kigoma dhidi ya Simba Queens ya Dar es salaam.

"Tukimaliza Grassroot kwa watoto tutaanza pilika kwa mechi za wamama ambapo ufunguzi wa Super 8 tunatarajia Mgeni rasmi awe Waziri wa Habari, sanaa, utamaduni na Michezo Harrison Mwakyembe,  " amesema.

No comments