MASHINDANO YA KUOGELEA KUANZA RASMI MARCH 24 JIJINI DAR ES SALAAM.




Mashindano ya Taifa ya mchezo wa Kuogelea yanatarajia kufanyika Machi 24 na 25 mwaka huu Katika bwawa la Shule ya IST jijini Dar es Salaam kwa kushirikisha waogeleaji watakaoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola.


Katibu Mkuu wa chama cha kuogelea nchini (TSA) Ramadham Namkoveka amesema,  lengo la kuwaalika waogeleaji hao ni kuweza kuwaweka fiti kwaajili ya kuiwakilisha nchi katika Michuano ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Aprili mwaka huu nchini Australia. 

"Mashindano haya ni ya siku mbili na tumewaalika wachezaji wetu walio ndani na nje ya nchi na hasa wale watakaoshiriki jumuiya ya madola kuona wamefikia wapi katika upande wa maandalizi, " amesema. 

"Tumeshatuma mwaliko kwa wachezaji wote na Tarehe 16 itakuwa ndio mwisho wa kithibitisha kushiriki, kwahiyo tunaimani kabisa mashindano haya ambayo yanafanyika mfululizo yataleta msisimko kwa washiriki na kuweza kuboresha muda wao zaidi, " amesema. 


Namkoveka ameongeza kuwa katika mashindano hayo pia watachagua waogeleaji wa kuunda timu ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya Dunia yatakayofanyika Desemba mwaka huu nchini China. 

"Wachezaji watakaofanya vizuri katika mashindano haya watapata nafasi ya kuteuliwa katika timu ya Taifa kwahiyo sio kwaajili ya Jumuiya ya Madola, tunamahitaji mengi tunapoandaa mashindano ya Taifa kwahiyo tunatarajia wachezaji kutoka klabu zote wataweza kushiriki maahindano haya, " amesema.

Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.

No comments