MECHI ZA MAJARIBIO NI CHACHE LAKINI TUPO TAYARI KUPAMBANA NA DR CONGO KUWANIA KUFUZU AFCON 2019 NIGER - WACHEZAJI NGORONGORO HEROES

Mara baada ya kumaliza michezo yake miwili ya Kimataifa ya Kirafiki, Kikosi cha Ngorongoro Heroes kimesema japo wamepata maandalizi ya muda mfupi lakini wapo tayari kwaajili ya kupambana na DR Congo katika mchezo wa kwanza wa kuwania kufuzu kushiriki Fainali za AFCON U20.


Nahodha wa Kikosi cha Ngorongoro Heroes Dickson Job amesema, mechi mbili bado hazijatosha kwaajili ya maandalizi lakini mazoezi na maelekezo ya Kocha yataweza kuwapa muongozo ili kuhakikisha wanafuzu na kuweza kushiriki AFCON mwakani nchini Niger.

Tumejiandaa vizuri na tupo tayari kwa mechi dhidi ya Congo, kwa mechi mbili kiukweli hazijatosha lakini inatibidi na hii ni kutokana na kutokuwa na muda mrefu wa maandalizi ila tunaendelea kujipanga na ninaimani tutafanya vizuri katika mchezo huo na kusonga mbele zaidi, ” amesema.

Job amewaomba watanzania kuendelea kuwapa sapoti kama ilivyokuwa katika kikosi cha Serengeti Boys kwani wanaamini wataweza kuwapa furaha watanzania.

Kwaupande wo washambuliaji wa Kikosi hicho Muhsin Malima na Abutwalib Msheri wamesema wapo imara kwaajili ya kuhakikisha wanalitetea pamoja na kulitangaza Taifa kupitia Soka huku wakiongeza kuwa wanajua wanadeni kubwa kwa watanzania hivyo watapambana ili kuhakikisha wanafanikisha kile walichokusudia.

Mechi tulizocheza ni kipimo kizuri lwaajili ya maandalizi ya mchezo unaofuata ambao niwakuwania kufuzu AFCON na tunawaahidi watanzania kuendelea kufanya vizuri na tunawaomba waendelee kuja kutupa sapoti, ” amesema Muhsin Malima.

Muhsin amewataka Watanzania kutokukata tamaa kwani bado wapo imara na wanaendelea kupambana huku wakitunza mazoezi wanayoyapokea kutoka kwa Kocha na imani yao ni kuweza kufanya vizuri zaidi katika kila mechi.

Tunafuata maelekezo ya Kocha na Kila mchezaji anaijua nafasi yake katika mchezo unaofuata hivyo tunaamini tutapambana kwaajili ya kuhakikisha tunashinda, ” amesema Abutwalib Msheri.

Msheri amesema, Kikosi kilichopo kambini ni mchanganyiko wa Serengeti Boys iliyopita na wachezaji wengine ambao hawakuwa kwenye kikosi hicho na hapo awali ilikuwa nguvu kuelewana katika mazoezi lakini kwa sasa wapo pamoja na wachezaji wote ni wamoja na lengo lao pia ni moja kwani mazoezi ya Kocha yameweza kuwaunganisha ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.


Kikosi cha Ngorongoro Heroes

No comments