WAOGELEAJI 150 KUSHIRIKI MASHINDANO YA TAIFA KESHO BWAWA LA SHULE YA KIMATAIFA YA TANGANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Waogeleaji takribani 150 kutoka Klabu 12 zilizopo hapa nchini wanatarajia kushiriki mashindano ya Taifa yatakayoanza kesho na kuhitmishwa Jumapili ya Machi 25 katika Bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika jijini Dar es salaam.


Katibu Mkuu wa Chama cha kuogelea nchini (TSA) Ramadhan namkoveka amesema, katika Klabu hizo zipo Klabu tatu kutoka visiwani Zanzibar huku akiongeza kuwa wachezaji waliokuwa nje ya nchi kwaajili ya masomo ambao pia wanajiandaa a mashindano ya Jumuiya ya Madola wameshawasili akiwemo nahodha wa timu ya Taifa Hilal Hilal.

Wachezaji takribani 150 watashiriki mashindano haya kutoka klabu 12 za hapa Tanzania ikiwemo klabu Tatu kutoka Zanzibar ambazo ni Wahuu, KMKM na JKU pia wachezaji ambao wapo nje ya nchi kwaajili ya masomo na ambao tunatarajia pia watashiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola, tayari Nahodha Hilal Hilal ameshawasili, Sonia Tumiyoto, Colins Saliboko, Philips Partick na wachezaji wengine wanawasili hii leo, ” amesema.

Namkoveka amesema, wanatarajia kuwa a waamuzi zaidi ya 40 wanaofahamisha na shirikisho la mchezo wa kuogelea ulimwenguni (FINA) wakiwemo Khalid Lushaka, Noel Kihunsi, Samson Makere pamoja na Samson Kimimba.

Namkoveka ameongeza kuwa katika mashindano ya Taifa pia watapata wachezaji watakaofuzu kushiriki mashindano ya 14 ya Kimataifa yatakayofanyika Desemba 11 mpaka 16 mwaka huu nchini China.

Mashindano haya pia tutayatumia katika kufuzu kwaajili ya mashindano ya Kimataifa ya 14 yatakayofanyika Hangzhou nchini China na ambayo tumepata Baraka kutoka FINA, kwahiyo vigezo vya kuchagua wachezaji pia vipo vingi ambavyo tunaamini vitatusaidia kuweza kupata wachezaji wazuri zaidi, ” amesema.

No comments