TIMU YA TAIFA YA KRIKETI YA WANAUME KUANZA KAMBI MEI MAANDALIZI MICHUANO YA AFRIKA U19 ITAKAYOFANYIKA AFRIKA KUSINI MWAKA HUU

Mara baada ya kupata wachezaji takribani 10 watakaoboresha kikosi cha Timu ya Taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 19 wa mchezo wa Kriketi ambacho kinajiandaa na Michuano ya Afrika, Kikosi hicho kinatarajiwa kuanza kambi mwanzoni mwa Mwezi Mei kikiwa katika makundi.

Mratibu wa Timu za Taifa za mchezo wa kriketi hapa nchini Hamis Abdallah amesema, wamefanikiwa kupata wachezaji takribani 10 ambao watafanya idadi ya wachezaji wa timu hiyo kuwa 24 ambao watakuwa Katika kambi za mikoani kabla ya kukutana mwezi Juni kwaajili ya Kambi rasmi ikiwa ni maandalizi ya mwisho kabla ya kuelekea Afrika kusini kwaajili ya mashindano hayo yatakayoanza mwezi Agasti mwaka huu. 

"Baada ya kumaliza mashindano ya mkoa wanachama ambayo tuliyaandaa kwaajili ya kutafuta wachezaji ambao watafanya maboresho kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ambayo itaanza maandalizi ya U19 Afrika,  baada ya kuwapata vijana hao tumewapa mapumziko na mwanzoni mwa mwezi Mei wataanza kambi, " amesema. 

Hamis amesema,  kutokana na ratiba ya mashindano ambayo yanatarajiwa kuanza wiki ya Tatu ya mwezi Agasti, Kikosi kitakuwa katika kambi ya pamoja kuanzia Mwezi Juni mpaka wiki ya Kwanza ya mwezi Agasti ambapo watachagua kikosi kamili ambacho kitaelekea nchini Afrika kusini kwaajili ya michuano hiyo.


Kriketi

No comments