SABABU ZA KOCHA WA NGORONGORO HEROES KUCHAGUA WACHEZAJI 28 BADALA YA 30 KATIKA KIKOSI HICHO HIZI HAPA.
Benchi la ufundi la Timu ya Vijana
wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) limefanya mchujo na kupata
wachezaji 28 kati ya 43 waliokuwa kambini kwaajili ya maandalizi ya michezo ya
kuwania kufuzu AFCON U20 itakayofanyika mwakani nchini Niger.
Kocha msaidizi wa Ngongoro Heroes
Oscar Milambo amesema, kikosi walichokipata kitacheza mchezo wa kwanza wa
kirafiki mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Morocco lengo likiwa ni kuwaangalia
nikwanamna gani wanaweza kujiandaa kwenda kwenye hatua ya kufuzu ambapo mchezo
wa kwanza watacheza na DR Congo huku akielezea sababu za kuchagua vijana 28
badala ya 30 kama walivyopanga hapo awali.
"Mara baada ya mchujo tutakuwa
na mechi ya Kirafiki siku ya Jumamosi dhidi ya Morocco hapa nyumbani, kwahiyo
vijana 28 ndio watakaoendelea na maandalizi ya moja kwa moja na mchezo na
Morocco utakuwa wa kwanza kuwaangalia wakishindana na vijana wenye umri sawa na
wao ili kuona ni kwamna gani sasa tunaweza kujiandaa, " amesema.
Kocha Milambo amesema, hapo awali
walikuwa na lengo la kubaki na vijana 30 lakini vigezo walivyotumia kutafuta
vijana hao ndivyo vilivyochangia kupata vijana pungufu.
"Kwanini vijana 28 nasio 30?
Vigezo tulivyotumia kufanya mchujo havijapatikana kwa wengine ndio maana
tumepata vijana hawa 28 na hatukuona sababu ya kulazimisha kuongeza kwasababu
kwamuda wa maandalizi tulionao wasingeweza kwenda sawa na kasi ya ubora wa
wachezaji hawa 28 waliopatikana, " amesema.
Oscar amesema, wanaamini kuwa timu
hiyo inayoundwa na vijana walioshiriki AFCON U17 itafanya vizuri katika
mashindano hayo kutokana na uzoefu walionao
Kwaupande wake Kocha wa Magolikipa
wa Timu hiyo Peter Manyika amesema, kwaupande wake anaimani na walinda mlango
watatu waliopatikana katika mchujo huo na kwamuda uliopo wa maandalizi
utasaidia kufanya marekebisho ya makosa watakayoyaona ili kuweza kufanya vizuri
katika nafasi walionazo.
"Wakati wa mchujo kulikuwa na
changamoto lakini tumeweza kupata magolikipa ambao tunaamini ni wazuri na
wanafuata maelekezo kwa umakini hivyo tunaamini watafanya vizuri, "
amesema.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Post a Comment