MAAMUZI YA FA KWA ROBERTO FIRMINO JUU YA TUHUMA YA KAULI YA KIBAGUZI.

Chama cha soka nchini England (FA) kimetoa taarifa na kusema kwamba mshambuliaji wa klabu ya Liverpool Roberto Firmino hana hatia juu ya lugha aliyotumia dhidi ya mchezaji wa Everton Holgate Mason  kutamka maneno ya kibaguzi  ndiyo inaelezwa kuleta utata kwa mwamuzi  pamoja na Holgate Mason licha ya kuwa Firmino alitoa maneno hayo kwa kutumia  lugha ya Kireno.


Katika hali ya kawaida inahitajika utulivu wa hali ya juu pindi linapotea jambo la ubaguzi wa rangi katika nchi ya England hivyo chama cha soka nchini humo FA kililazimika kumshirikisha mtaalam wa lugha ya Kireno kwa dhamira ya kutambua maana halisi ya kile kilichozungumzwa na Firmino.

Dhidi ya mchezaji mwenzake wa Everton na kugundulika kuwa maana ya maneno au matamshi hayo kwa mujibu wa mtaalam huyo ameyatambua matamshi hayo hivyo alifuatilia jinsi Firmino alivyochezesha mdomo wake wakati akiongea na Holgate.

Hata hivyo mtaalam huyo amesema kwamba ukiangalia jinsi Firmino alivyoongea unaweza kusema kuwa ni mtu mwenye uzoefu wa kutamka  matusi ya ubaguzi wa rangi katika maisha yake hivyo maneno aliyotamka Firmino kwa mujibu wa mtaalamu ni kwamba alimwambia Holgate “kaa kimya unajua ni jinsi gani maumivu nimeyapa nyuma ya mgongo“ alisema mtaalam huyo mara baada ya uchunguzi zaidi.

Ni takribani miezi miwili sasa imepita baada ya kudaiwa kumtolea kauli ya kibaguzi mchezaji wa klabu ya Everton inayoshiriki ligi kuu soka nchini England Mason Holgate.

No comments