WENGER HANA MPANGO WA KUONDOKA ARSENAL KABISA

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema katika maswali yanayomfurahisha ni yale yanayohusu hatima yake ndani ya timu hiyo ambayo ameifundisha tangu mwaka 1996. 


Kocha huyo raia wa Ufaransa amesema kama kuna kitu hakimuwazishi ni nafasi yake ndani ya Arsenal licha ya kupoteza mechi sita kati ya 12 ndani ya mwaaa 2018 ndio mana huwa anafurahia maswali yanayouliza hatima yake.

''Siwazii mkataba kwasasa zaidi nafikiria namna ya kuifanya timu iwaze mchezo wa kesho'', amesema Wenger kuelekea mchezo wa EPL kesho dhidi ya vinara Manchester City.

Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 68 alisaini mkataba mpya wa miaka miwili mwezi Mei 2017 licha ya kushindwa kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika miaka 20.

No comments