BMT YASITISHA UCHAGUZI WA SHIRIKISHO LA NGUMI NCHINI.



Baraza la Michezo nchini (BMT) limesitisha uchaguzi wa Shirikisho la ngumi nchini (BFT) uliotakiwa kufanyika Jumamosi ya Ferbruari 24 mjini Dodoma mara baada ya kukuta kasoro ndani ya katiba ya shirikisho hilo. 


Afisa habari wa BMT amesema mara baada ya kukutana na kasoro hizo, Katibu Mkuu Mohamed Kiganja aliunda kamati yenye wajumbe sita ambao wamepewa majukumu ya kuhakikisha wanarekebisha katiba ikishirikiana na Serikali ndani ya miezi mitatu. 

"Kamati hiyo imepewa majukumu yakurekebisha katika ili iweze kwenda sawa na shirikisho ikiwa ni pamoja na kuwa na dhumuni,  na ndani ya miezi hii mitatu wahakikishe wanaandaa mkutano mkuu wa uchaguzi na katika mkutano huo wahakikishe kwamba ili kuwapunguzia gharama wanachana ambao ni wapiga kura wahakikishe wanawapunguzia mzigo kwa kushirikiana na Baraza, watafute pesa kwaajili ya kuwasaidia katika uchaguzi utakaofanyika hapo baadae, " amesema. 

Najaha amesema, katika kamati hiyo iliyochini ya Rais wa BFT Mutta Rwakatare imetakiwa kuyafanyia kazi Yale yote waliyoelekezwa ikiwa ni pamoja na kulenga katika katiba kunakuwa na kanuni za uchaguzi, ufundi na utawala ili kuhakikisha shirikisho hilo linasonga mbele.

Najaha amemaliza kwa kutoa wito kwa Vyama na maahirikisho kuhakikisha katiba zao zinakuwa na vigezo na kuwa na mazoea ya kupeleka katiba kwa msajili ili katiba ziweze kufanyiwa marekebisho pale panapostahili.

No comments