HIKI NDICHO KINACHOSUBIRIWA NA BMT KABLA YA KUTOA TAMKO KUHUSU KUFUNGIWA KWA MAKAMU WA RAIS WA TFF KUTOKUJIHUSISHA NA SOKA

Mara baada ya Kamati ya maadili ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kumfungia maisha kutokujihusisha na masuala ya Soka aliyekuwa Makamu wake Michael Wambura, Baraza la Michezo nchini (BMT) limesema, bado halijapokea barua kutoka kwa shirikikisho hilo kuhusiana na maamuzi hayo.

Katibu Mkuu Mkuu wa BMT Mohamed Kiganja amesema, kwa sasa ni mapema mno kulizungumzia suala hilo kwani mpaka sasa hawajapewa chochote kile zaidi ya kusikia kwenye vyombo vya habari.

Mpaka sasa sisi kama serikali hatujapewa chochote kuhusiana na suala hilo kwahiyo sio rahisi kuzungumzia kitu ambacho unakisikia kwenye mitandao na kwenye vyombo vya habari hivyo hatuwezi kutoa maelekezo yoyote, ” amesema.

     
Katibu Mkuu wa BMT, Mohamed Kiganja
                                                 

Kiganja amesema, suala lililotokea TFF halina pande moja hivyo wanasubiri TFF waieleze serikali walipoanzia mpaka walipoishia na hata Wambura pia ambapo mara baada ya kupata pande zote mbili ndipo watatoa tamko kama itatakiwa.

Kiganja amesema, jambo lililotokea ni kubwa na halipaswi kukaliwa kimya na limeshtua Watanzania, wadau wa Soka na hata nchi kwa ujumla.

Wambura amefungiwa kutokujihushisha na soka kwa makosa matatu ya kupokea fedha za TFF malipo yasiyo halali, kugushi barua na kushusha hadhi ya TFF. 


Aliyekuwa Makamu wa Rais wa TFF, Michael Richars Wambura

Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
       

No comments