ROGER FEDERER AMEPIGA MKOREA NA KUTINGA HATUA YA NUSU FAINALI INDIAN WELLS.
Mchezaji tennis, Roger Federer amefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali
ya michuano ya Indian Wells na kuendelea kulinda heshima yake ya kuwa
namba moja kwa viwango vya ubora duniani.
Federer amefanikiwa kutinga hatua hiyo siku ya hapo jana siku ya
Alhamisi usiku baada ya kumshinda Mkorea Kusini, Chung Hyeon kwa jumla
ya seti 7-5 6-1.
Mchezaji huyo mwenye umri mkubwa zaidi katika tennis anatarajia
kukutana na Borna Coric, ambaye amemfunga Kevin Anderson kwa seti 2-6
6-4 7-6.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Post a Comment