SERENGETI BOYS KUTUPA KARATA YAO YA KWANZA DHIDI YA UGANDA JUMAPILI, MICHUANO YA CECAFA U17 BURUNDI
Kikosi cha wachezaji 20 cha timu ya Taifa ya Soka la vijana
walio na umri chini ya miaka 17 "Serengeti Boys" kilichoondoka hapo
jana kuelekea nchini Burundi kwaajili ya michuano ya CECAFA inayoanza
kutimua vumbi hapo kesho, Jumapili kinatarajia kutupa Karata yake ya
kwanza dhidi ya Uganda.
Afisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Clifford
Ndimbo amesema, maandalizi bora waliyoyatoa kwa wachezaji wanaounda
kikosi hicho ikiwemo mechi za kirafiki wanaamini wataipeperusha vema
bendera ya Tanzania katika michuano hiyo ambayo ni sehemu ya maandalizi
ya michuano ya AFCON U 17 itakayofanyika mwakani Tanzania ikiwa ni nchi
mwenyeji.
"Kikosi kimeondoka vizuri kikiwa na imani kubwa ya kufanya
vizuri katika mashindano hayo ambayo yanaanza kesho lakini Tanzania
itatupa karata yake ya kwanza siku ya Jumapili, " amesema.
Ndimbo amesema, waliwaandalia mazingira ya kwenda kufanya
vizuri vijana hao kwa kwa na mechi mbalimbalï za kirafiki dhidi ya
vijana wenye umri sawa na wao ambapo waliweza kuonyesha kiwango kizuri.
Michuano ya CECAFA inashirikisha timu nane zikiwa katika
makundi ambapo kundi A kunatimu za Somalie, Ethiopia, Burundi na Kenya
huku kundi B kukiwa na timu za Tanzania, Sudan, Zanzibar na Uganda.
![]() |
Serengeti Boys |
Post a Comment