SINGIDA UNITED YAFURAHISHWA KUONDOKA KWA KOCHA MHOLANZI
Uongozi
wa Klabu ya Singida United umesema unajisikia fahari kuona baadhi ya
Vilabu vikubwa vya Soka ndani na nje ya nchi kumuhitaji Kocha wao
Mholanzi,
Hans
van der Pluijm kwani wanaamini ni Kocha mkubwa na wenye uwezo ndio
maana vilabu hivyo vimemtolea macho kuhitaji huduma yake.
Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga amesema bado wanamkataba na
Kocha Hans lakini iwapo utafika wakati wa kuondoka hawawezi kumzuia
kwani ni kazi yake na hawatakuwa na tatizo na Klabu yoyote
itakayomuhitaji.
“Sisi tunaona ni fahari, unajua ukiona Klabu ndogo lakini ni kubwa
kwamaana imeingia kwenye Ligi kuu msimu huu na inakocha mkubwa kama
Hans na vilabu vikubwa vinamuhitaji, kwanza tumepokea ofa nyingi
kutoka Marekani, na pia kuna Klabu kutoka Sudan wakimuhitaji lakini
vipo vilabu vikubwa hapa nchini vinamuhitaji, sisi ni heshima kwetu
kwamba ni moja kati ya Klabu ambayo vilabu vikubwa vinaweza
kuiangalia na kumuhitaji Kocha, ” amesema.
“Sisi Hans bado tunamkataba naye lakini tunaamini kabisa anaweza
kuondoka kwasababu hivi vilabu vimekuwa na nguvu kubwa sana ya
kumuhitaji, lakini Hans bado anamapenzi na Singida United, ila sisi
hatuwezi kumzuia kwasababu yeye pia anatafuta riziki kupitia kazi
yake, kwahiyo kikubwa ni kwamba Hans kwa sasa anayemuhitaji sisi
hatuna tatizo, ” amesema.
Sanga ameongeza kuwa kuelekea katika muendelezo wa Ligi kuu wakiwa
wamebakisha mechi tano ambapo kesho watakuwa ugenini wakipambana na
Mbeya City kikosi kimejipanga kuhakikisha kinaendelea kulinda heshima
ya Timu na pia kuhakikisha wanatimiza lengo lao la kusalia katika
nafasi za juu mwishoni mwa msimu wa Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara.
“Tunapambana ili kwenye Ligi kuu historia yetu iweze kubaki kuwa
salama kwamaana tunahitaji kuwa kwenye nafasi nne, tatu au mbili na
hilo linawezekana kwasababu mpira unadunda na bado tunamechi tano
kabla ya kumaliza Ligi kwahiyo hauwezi jua kitakachotokea, ”
amesema.
“Tunaenda kucheza na Mbeya City tukiwa tunawaheshimu kwani wametoka
sate na timu kubwa kama Yanga hivyo naamini hata sisi wametupania na
pia wanahitaji kujiondoa katika nafasi waliyopo, lakini sisi sio
ngazi ya wengine kung'ang'ania kutokushuka daraja, sisi tunacheza
mpira na hatuingii Uwanjani kumpa mpinzani wetu pointi tatu bali
tunapambana, ” amesema.
![]() |
Kocha wa Singida United,, Hans van der Pluijm |
Post a Comment