GENNARO GATTUSO KATIKA UBORA WAKE NDANI YA AC MILAN.
SIKU moja katika viwanja vya mazoezi
AC Milan, Gennaro Ivan Rino Gattuso aliyesimama hatua chache alikokuwa Andrea
Pirlo, alimfuata na kumwambia hajioni kama anastahili kuitwa mchezaji, ila
Pirlo anastahili kuitwa jina hilo.
Gattuso alimwambia Pilro kila
akimtazama anajiona yeye angefaa kufanya shughuli nyingine, lakini sio kucheza
soka.
Hatimaye wawili hawa wametundika
daruga. Pirlo anaenda kustahafu mwishoni mwa msimu huu, Gattuso amekuwa kocha
wa AC Milan klabu aliyochezea kwa mafanikio.
Aliwahi kusema mwanafalsafa wa
Kijerumani Kahl Henrik Max kuwa nyakati ngumu hupita, lakini watu wagumu
hawapiti.
Gattuso ni mtu mgumu aliyerudi
uwanjani. Wakati huu akirudi kama kocha, si mchezaji tena. Amerudi kibabe
kama alivyoondoka kibabe.
Wakati anatangaza kung'atuka
Jiji la Milan na kuungana na familia yake alitoa machozi kama ya Simba
aliyefiwa na mtotowe. Hakuna aliyeona wala kujali thamani ya machozi yake zaidi
ya moyo wake wa chuma uliomwagiwa damu za kikatili za Kiitaliano.
Max alipowasema watu wagumu hawapiti
alimaanisha watu aina ya Gattuso. Hawa ni watu wachache wenye mioyo ya ubondia,
lakini waliamua kubeba njumu na kuja uwanjani kucheza soka.
Gattuso mtemi, mgomvi, katili asiye
na chembe za huruma ndiyo kocha wa AC Milan hivi sasa. Ameichukua timu katika
mazingira magumu na mwenyewe akisema anataka kurudisha heshima yao ndani ya
Italy na ulaya kiujumla.
Kando ya mbinu zake kuwafikia
wachezaji na wachezaji kuzitekeleza kifasaha, moyo wake mgumu umeanza kuwaingia
wachezaji.
Milan inapambana siku hizi.
Wachezaji wanacheza kwa moyo mmoja. Wanacheza kana kwamba hawachezi tena mechi
nyingine.
AC Milan ya mwisho kuwa na passion
hii ni ile ya kocha Massimiliano Allegri, lakini AC Milan nyingine hazikuwa
zikijua thamani na uzito wa jezi wanaovaa na timu wanayochezea.
Wiki iliyopita Gattuso na vijana wake
walienda uwanja wa Stadio Olympic kucheza dhidi ya AS Roma na kuibuka na
ushindi wa mabao 2-0.
Katika mpira mmoja wa kurusha beki
wa Roma
Aleksandar Kolarov alikutana na domo
chafu la Gattuso.
Kolarov ameeleza kuchukizwa na kauli
chafu zilizotolewa na Gattuso juu yake.
Kolarov amesema kuwa wakati
akijiandaa kurusha mpira dakika ya 35 kipindi cha kwanza alibughuziwa na
Gattuso kwa maneno ya kejeli ambayo hakutarajia maneno kama hayo kutoka kwenye
kinywa cha Gattuso.
"Alinifuata huku akiniambia kuwa
nina bahati sikucheza soka kipindi ambacho yeye alikuwa uwanjani, kwa maana
kipindi chake hakukuwa na warembo kama mimi wenye maumbile ya kuvutia na kutia
hamasa"
alisema Kolarov.
Nimeshangaa kitu hapa. Gattuso
anatuambia Kolarov ni kama mwanamke mrembo anayeweza kumvutia mwanaume kama
yeye, hapa alimzungumzia Kolarov yupi, yule aliyewahi kupita Manchester City au
yupi?
Kolarov mbishi kimtazamo, kiugumu na
mwenye madhara langoni mwa adui, Gattuso alimaanisha Kolarov yupi?
Kama ugumu wote ule wa Kolarov bado
Gattuso anataka kutuaminisha anachokiamini kuhusu Kolarov, vipi siku timu yake
ikicheza dhidi ya Neymar?
Gattuso hakumfanyia fair Kolarov.
Lakini shida ya Gattuso mwenyewe hajali, mara zote ni mtu wa kusema
anachokiamini. Muda huu tunaotumia kuitafakari kauli yake ya kijinga kabisa,
tufahamu kuwa Gattuso ndiyo yuko hivi. Alianza kutuonyesha ujinga wake wakati
anacheza, wacha leo hii aendelee kutuonyesha wakati akifundisha
Post a Comment