UONGOZI MBAO FC WASHANGAZWA NA MATOKEO YA VPL,WAKANUSHA KUTOKUWALIPA WACHEZAJI MISHAHARA.
Mara baada ya kupoteza michezo minne
mfululizo ikiwemo wa jana ambao walipoteza dhidi ya Azam FC kwa bao 2-1 Klabu
ya Mbao FC imesema bado inashangazwa licha ya pointi walizonazo lakini hawapo
nafasi ya mwisho hivyo wanaamini hawawezi kushuka daraja.
Mwenyekiti wa Mbao FC Solly Njashi
amesema, kufungwa ni sehemu ya mchezo na pia imechangiwa na safari nyingi
ambazo zimesababisha uchovu kwa wachezaji lakini wanahitaji kuongeza nguvu ili
kufanya vizuri kwa michezo iliyobakia.
"Mimi kitu ambacho
kinanishangaza ni kwamba tumefungwa michezo mingi sana lakini bado hatujawa wa
mwisho, na naimani kabisa kama tumemaliza mechi ya jana na hatujawa wa mwisho
na mizunguko tuliyokuwa nayo basi naimani tunakwenda kufanya vizuri na
mashabiki wetu waendeleze umoja, " amesema.
"Kufungwa ni sehemu ya mchezo
kwasababu katika soka huwezi kwenda na matokeo yako mkononi, unaenda kupambana
Uwanjani lakini mkumbuke kwamba mechi za ugenini zinakuwa ngumu na inachangiwa
na safari nyingi, " amesema.
Njashi amesema, bado
wanavijana ambao umri wao bado haujawa vizuri katika kupambana na mechi za
ugenini zinawasumbua hivyo wanaamini bado wanamuda wa kuongeza nguvu ili
kushinda mechi zinazofuata.
Wakati huohuo Njashi amekanusha
suala la kutolipwa mishahara kwa wachezaji ndio liachangia timu kutofanya
vizuri ambapo ameongeza kuwa ni miezi miwili pekee ndio hawajawalipa wachezaji
na kauli hizo zinazotolewa na baadhi ya wadau wa soka haziwezi kufelisha
mikakati yao ya kuiweka timu katika sehemu imara zaidi.
"Changamoto ya mishahara ni
sehemu ya timu nyingi na sio Mbao pekeyake utakuta hata timu kubwa zipo kwenye
changamoto hizi, na katika mpira wetu inaeleweka wazi kwamba tunaendesha katika
utaratibu upi, na Mbao hatujawalipa wachezaji wetu kwa miezi miwili na
tumejitahidi sana na tutaendelea kupambana na hilo kuhakikisha kwamba haliwezi
kutokea, " amesema.
"Labda nizungumze tu, kunakauli
nyingi zinatoka lakini nadhani kunawatu wanamikakati yao juu ya Timu ya Mbao
lakini nasema wazi hawatakaa waifelishe kwamipango tuliyonayo sisi, na naimani
sisi hatuwezi kusikiliza nani anasema nini ila tumesimama kwenye mipango yetu
tuliyonayo kuhakikisha kwamba Mbao tunaitoa hapa ilipo kwenda mahala kwingine,
" amesema.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Follow us on Instagram @Tiktaktz ili uwe wa kwanza kupata taarifa mpya za michezo yote ndani ya nchi na nje ya nchi.
Post a Comment